Waziri wa Habari Vijana na Michezo Mhe. Emmanuel Nchimbi amepata ajali ya gari maeneo ya Kibaigwa Mkoani Dodoma, baada ya kugongana na basi la abiria la Happy Nation. Waziri yuko salama ila gari lake limeharibika na hakuna abiria wa basi aliyepoteza maisha. Mhe Nchimbi alikua akisafiri na gari lake akielekea bungeni ambako kesho vikao vinaanza rasmi.
More at globalpublishers.info
No comments:
Post a Comment